Watu 10 wamekufa
na wengine 10 kujeruhiwa baada ya basi dogo la abiria walilokuwa wakisafiria
kugonga lori lililokuwa na kokoto lililoegeshwa kando ya barabara kasha kupinduka
katika eneo la Nyamhongholo, jijini Mwanza.
Akizungumza na
waandishi wa habari katika hospitali ya Rufaa ya Bugando, Daktari wa Idara ya
Dharura, Dk Regina Mutayangulwa, alisema miili ya abiria hao na majeruhi ilipokewa hospitalini hapo juzi usiku.
Majeruhi
waliolazwa katika wodi za upasuaji ni pamoja na wanawake watatu waliolazwa
katika wodi namba 9C na wanaume saba waliolazwa katika wodi namba 6Cna 8E na
hali zao zinaendelea vizuri.
Waliojeruhiwa ni
pamoja na Verynice Protas (22), Rosemary Petro (26), Prisca Peter (25), Hamad
Haruna (22) ambaye amevunjika mkono wa kushoto na paji la uso kuharibika na
Benson Joseph (27).
Wengine ni
Nyanda Sahani, Magesa Musa (30), Rushinge Nyerere, Japhet Mlangwa (23) na Shija
Nyanda Ngwenda.
Akizungumzia
ajali hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Valentine Mlowola, alisema
ilitokea Mei 13 saa moja usiku katika Barabara Kuu ya Mwanza- Musoma.
Alisema ajali
hiyo ilihusisha gari lenye usajili namba T 769 CQE aina ya Toyota Coaster,
lililokuwa likiendeshwa na Yohana Mayandakia likitokea Mwanza kwenda Bunda,
ambapo liligonga namba Lori aina ya Iveco, lenye namba T832 AEF na tela namba T 187 AEF.
Alisema lori
hilo lilikuwa limeegeshwa pembeni mwa barabara na dereva aliyeitwa Emmanuel Zakaria
(33) ambalo lilikuwa bovu.
Kamanda Mlowola
alisema chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva kutokuwa mwangalifu na ishara
iliyokuwa imewekwa mbele ya gari lililokuwa bovu. Dereva wa lori anashikiliwa
Polisi kwa uchunguzi zaidi.
No comments:
Post a Comment