Balozi
wa Misri nchini ametoa msaada wa vifaa vya upasuaji katika Hospitali ya Taifa
Muhimbili vyenye thamani ya Sh milioni 400.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Hospitali hiyo, Dk Marina Njelekela, alisema hayo katika hafla fupi
ya kupokea vifaa hivyo iliyofanyika hospitalini hapo.
Alisema
msaada wa vifaa hivyo, umefika wakati muafaka ambapo Serikali kupitia Wizara ya
Afya na Ustawi wa Jamii inatekeleza mkakati wa kuboresha na kuimarisha huduma
za afya.
Aliongeza
kuwa vifaa hivyo vitasaidia wagonjwa hasa wale wanaoandaliwa kwenda kufanyiwa
upasuaji walioko chumba cha upasuaji na wale wanaohitaji uangalizi maalumu
baada ya kufanyiwa upasuaji.
Pia
alisema katika Hospitali ya Taifa Muhimbili zaidi ya asilimia 60 ya wagonjwa
wanaohitaji huduma ya upasuaji ni wenye matatizo ya urolojia kwa hiyo huduma
hii ni muhimu sana hapa nchini.
Huduma
ya urolojia hapa nchini inatolewa na baadhi ya hospitali za rufaaa lakini idadi
kubwa ya Wagonjwa wanaohitaji huduma hizo hupata matibabu katika Hospitali ya
Taifa Muhimbili na Hospitali ya Rufaa ya KCMC iliyopo Mkoani Kilimanjaro.
“Katika
Hospitali ya Muhimbili urolojia ilianzishwa rasmi mwaka 2008 chini ya Idara ya
Upasuaji lengo ni ni kuboresha huduma kwa wananchi” alisema Njelekela.
Alisema
huduma ambazo zimekuwa zikitolewa na kitengo cha urolojia ni pamoja na uvimbe
wa tezi dume, kuziba kwa njia ya mkojo kutokana na kovu, saratani ya
kibofu,saratani ya tezi la kiume na mawe kwenye figo.
Aidha
aliishikuru serikali serikali ya Misri kwa ushirikiano wake mkubwa na
Tanzania kwani wamekuwa wakipokea wataalamu kuja kukaa na wataalamu hapa nchini
ili kuwapa ujuzi zaidikatika maeneo mbalimabli ya huduma za kibingwana urolojia
pia aliomba urafiki huu na ushirikiano huu uzidi kuimarishwa siku hadi siku.
Naye
balozi wa Misri nchini, Hossam Moharam alisema wataendelea kuisaidia Muhimbili
kwa kuipatia vifaa tiba mbalimbali vya upasuaji na pia tutaendelea
kubadilishana uzoefu.
“Uhusiano
wetu ni wa muda mrefu na tutaendelea kushirikiana na kushikamana ili tuweze
kusaidia jamii na tutahakikisha tunaendelea kubadilishana ujuzi” alisema
Moharam.
No comments:
Post a Comment