Wanafunzi
wa shule za sekondari wilayani Bagamoyo, wametakiwa kusoma kwa bidii na kufanya
vizuri kwenye mitihani yao, kama wanataka kufanikiwa katika maisha yao, kwani
elimu ni mkombozi wa maisha ya binadamu.
Mwito
huo umetolewa hivi karibuni na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo
(Wama), Mama Salma Kikwete, wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na
wanafunzi wa shule za sekondari za Mandera na Mboga wilayani Bagamoyo mkoani
Pwani.
Mama
Kikwete ambaye pia ni mke wa Rais Jakaya Kikwete, alisema kama wanafunzi
hao watasoma na kufanya vizuri katika mitihani yao, watafanikiwa
kimaisha, watapata kazi na kuwasaidia ndugu zao na kupunguza tatizo
la umasikini ndani ya jamii zao.
“Mjenge
tabia ya kusoma kwa makundi, msione fahari kukaa nyumbani hasa mwisho wa wiki,
tumieni muda wenu wa ziada kusoma kwa pamoja, mchague viongozi wa makundi na
kila mmoja wenu awe na somo la kuwafundisha wenzake hii itasaidia kila mtu
kufaidika na mwenzake,” alisema Mama Kikwete.
Mwenyekiti
huyo wa Wama aliwaasa wanafunzi wa kike, kutokubali kudanganywa na wanaume na
kujiingiza katika uhusiano wa kimapenzi wangali wanafunzi, kwani kufanya hivyo
watapata mimba zisizotarajiwa na ugonjwa wa Ukimwi, hivyo kukatisha masomo yao
na kutotimiza ndoto zao.
“Msikubali kudanyanywa na wanaume na
kujiingiza katika uhusiano wa kimapenzi wakati uko shule, hata kama mzazi wako
hana fedha za kutosha za kukupatia, usikimbilie kwa mwanamume.
“Unaweza
kutumia kipindi cha likizo kufuga kuku wa asili na unaporudi shuleni unawaomba
walezi wako wakuangalizie kuku hao wakikua utawauza na kujipatia fedha,”
alisema.
Kwa
upande wa walimu, aliwata kulea wanafunzi hao kama watoto wao wa kuwazaa kwani
wao ndiyo wenye dhamana kubwa katika malezi ya wanafunzi.
No comments:
Post a Comment