RAIS KIKWETE AMTUMIA SALAMU MFALME WA UHOLANZI

Rais Jakaya Kikwete amemtumia salamu za pongezi Mfalme wa Uholanzi, Willem Alexander kwa kutimiza umri wa miaka 47 jana.
Taarifa iliyotolewa jana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Mataifa, imemkariri Rais Kikwete akimhakikishia mfalme huyo kwamba uhusiano wa nchi yake na Tanzania utaendelea kuwepo.
“Ni furaha yangu, kwa niaba ya wananchi na Serikali ya Tanzania kukupongeza kwa kutimiza miaka 47,” alisema Rais Kikwete.
Aliendelea kusema, “wakati ukiendelea kusherehekea siku ya kuzaliwa kwako, nichukue nafasi hii kukueleza namna ninavyoridhishwa na uhusiano uliopo baina ya watu na nchi .”
Alimhakikishia kwamba Tanzania  itaendelea kufanya kazi naye pamoja na serikali yake kuimarisha uhusiano wa karibu na wa muda mrefu kwa faida ya pande zote.

No comments: