JWTZ WAKABIDHIWA VITABU KWA AJILI YA MAKTABA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amekabidhi vitabu 2,181 kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa ajili ya vyuo vya Jeshi ili kuongeza taaluma.
Alikabidhi vitabu hivyo  jana Dar es Salaam kwa Mkuu wa Majeshi, Jenerali Davis Mwamunyange na kuahidi kuendelea kutafuta vitabu zaidi kwa ajili ya kuboresha Maktaba ya Jeshi iliyopo katika Chuo cha Kijeshi kilichopo Monduli, mkoani Arusha.
Maktaba hiyo ilianzishwa na  Kikwete  alipokuwa mkufunzi katika chuo hicho miaka iliyopita.
"Lazima mtenge bajeti kwa ajili ya vitabu lakini na mimi nitaendelea kutafuta vitabu niwaletee ili kujijengea uwezo maktaba yetu ya Monduli,Ó alisema.
Akipokea vitabu hivyo kwa niaba ya Jeshi, Jenerali Mwamunyange amemshukuru Rais kwa juhudi zake za kuboresha Jeshi la Ulinzi  la Wananchi Tanzania kwa ujumla na kulifanya kuwa la kisasa zaidi.

No comments: