SHARO MILIONEA KUZIKWA MCHANA HUU KIJIJINI KWAKE...

Mwigizaji maarufu wa filamu nchini na msanii wa muziki wa kizazi kipya, Hussein Mkiety maarufu kama Sharo Milionea ambaye alifariki jana majira ya Saa mbili usiku kwa ajali ya gari iliyotokea mkoani Tanga, anatarajiwa kuzikwa mchana huu kijijini kwao Lusanga, wilaya ya Muheza. Sharo Milionea alikuwa akitoka Dar es Salaam kuelekea kijijini kwao kumsalimia mama yake ndipo akafikwa na ajali iliyochukua uhai wake. KUSHOTO: Mwili wa Sharo Milionea mara baada ya kufikishwa hospitalini. KATIKATI: Gari alilokuwa akisafiria Sharo Milionea likiwa eneo la tukio mara baada ya kupinduka na kuparamia mti. KULIA: Sharo Milionea enzi za uhai wake.
   ***HABARI ZILIZOTUFIKIA zinasema kwamba baada ya kikao cha familia, imeafikiwa kwamba Sharo Milionea sasa atazikwa kesho.***   

No comments: