MWIGIZAJI JOHN MAGANGA KUZIKWA MCHANA HUU MAKABURI YA KINONDONI...


      
PICHANI: Marehemu John Maganga (mwenye fulana nyeupe) katika kipande kilichompatia umaarufu cha filamu ya Mrembo Kikojozi.
Msanii wa filamu nchini, John Stephen Maganga aliyefariki dunia Jumamosi iliyopita katika Hospitali ya Muhimbili, Dar es Salaam anatarajiwa kuzikwa mchana huu katika makaburi ya Kinondoni.
Taratibu za mazishi zinafanyika nyumbani kwao Mwananyamala 'A' karibu na Baa ya KopaKabana ambako waombolezaji watapata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho.
Marehemu alijizolea umaarufu mkubwa hasa kwa jinsi alivyoigiza kwenye filamu ya Mrembo Kikojozi akicheza sambamba na Mtunissy, Aunt Ezekiel na Biggy Lumole Matovolwa.
John aliingia kwenye darasa la sanaa ya uigizaji mwaka 2001 akiwa chini ya walimu Thea na Deo Shija na ilipofika mwaka 2008 akaanza rasmi kuigiza.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi, Amen.

No comments: