BINTI WA MIAKA 11 ALIYEBAKWA BUSTANINI KUFANYIWA UPASUAJI...

Polisi wakiwa wamefunga lango kuu la bustani hiyo kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
Binti wa miaka 11 anahitajika kufanyiwa upasuaji baada ya mwanaume kumburuta kutoka mtaani na kumfanyia shambulio la ubakaji.
Mwanaume huyo alimfuatilia binti huyo, ambaye alikuwa kavalia sare za shule, baada ya kuwa ameshuka kwenye basi katika Mtaa wa Bury mjini Enfield majira ya Saa 11 jioni ya Ijumaa.
Polisi wanaendelea kuomba mashuhuda na taarifa kuhusu shambulio hilo huku wakifanya msako kumtafuta mwanaume huyo aliyeelezewa kuwa amefuga nywele ndefu nyeusi kwa mtindo wa afro, akiwa kavalia kizibao cha rangi ya kijivu nzito na suruali nyeusi ya jeans.
Baada ya kuhisi kuwa anafuatiliwa, binti huyo alivuka barabara ya Galliard kujaribu kumpoteza maboya mwanaume huyo.
Lakini alimburuta kwenye Bustani ya Jubilee katika uwanja na eneo la shimo la gofu na kisha kumshambulia kwa kumbaka.
Polisi walimwelezea mtuhumiwa huyo kama mwanaume mweusi aliyefuga nywele kwa mtindo wa afro akiwa kavalia kizibao cha kijivu na suruali nyeusi ya jeans.
Doria za Polisi zimekuwa zikirandaranda eneo hilo na Mpelelezi Inspekta Simon Ellershaw alisema: "Ni shambulio baya kwa binti wa miaka 11 asiye na ulinzi.
"Haihitaji kusema jinsi gani shambulio hili lilivyo la kutisha.
"Bado yuko hospitali na anatakiwa kufanyiwa upasuaji kutokana na majeraha aliyopata. Amekuwa akifarijiwa na familia yake na ninaamini ataweza kupona kabisa kwa hali ya kawaida."
"Anasema shambulio hilo lilitokea katika muda unaofahamika - yawezekana katika kipindi cha masaa mawili hadi matatu.
"Nawaomba waendesha magari, watembea kwa miguu na yeyote aliyekuwa kwenye bustani kati ya Saa 10:45 jioni na Saa 2 usiku, ambaye anaweza kuwa alimuona mwanaume akimfuatilia binti aliyekuwa kavaa sare za shule, kuwasiliana nasi.
"Kuna wakati alifahamu kwamba kuna mtu anamfuatilia, na akakatiza barabara mara kadhaa sababu ya hili.
"Kisha aliburutwa katika hifadhi na kufanyiwa shambulio la ubakaji.
"Alirejea nyumbani majira ya Saa 2 usiku na kulikuwa na utofauti kati ya wakati akipanda basi na pale anapofika nyumbani.
"Tunataka kuongea na sio yeyote ambaye alimuona mtu  aliyekuwa na mashaka katika eneo hilo lakini pia kama yeyote aliweza kuona binti mdogo wa shule aliyechanganyikiwa akizagaazagaa kwenye mitaa.
"Ni muhimu kuona kwamba tunamkamata mtu huyu."

No comments: