MAMA ADAI KUIBIWA MUME NA MWANAMKE MUUAJI...

KUSHOTO: Tracie anavyoonekana sasa baada ya kutoka jela. KULIA: Tracie akiwa na Lee Harvey.
Mama wa watoto wawili amesema mume wake aliibwa na mwanamke ambaye alimuua mchumba wake katika shambulio la kiwazimu la kisu.
Muuaji Tracie Andrews, ambaye alihukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kumchoma visu Lee Harvey mara 42 mwaka 1996, alimtongoza Phil Goldsworthy, kwa mujibu wa mke wake aliyejawa huzuni, Linsie.
Akizungumza na gazeti la The Sun, Linsie mwenye miaka 48 alisema Phil, baba wa watoto wanne alianzisha mahusiano na Tracie mwenye maiak 48, baada ya kukutana kwenye baa ambayo wote walikuwa wakifanya kazi.
Tracie alihamia katika nyumba za pwani ya kusini magharibi baada ya kuwa ameachiwa kutoka kifungoni mwaka 2011 baada ya kutumikia miaka 14 jela katika hukumu yake ya kifungo cha maisha.
Kwa sasa anatumia jina la Jenna Stephens na anafanya kazi ndani katika baa hiyo, ambako Phil anafanya kazi kama baunsa siku za Ijumaa usiku.
Linsie anadai Phil 'alivutiwa' na muuaji, ambaye anadaiwa kumlipia madeni yake ya Pauni za Uingereza 4,000, na kwamba angemlinda dhidi ya yeyote atakayemshutumu.
Alianza kurejea nyumbani 10 alfajiri baada ya zamu, akidai kulikuwa na kazi nyingi mno baa, na kukataa kufanya mapenzi, akidai Linsie alikuwa mnene sana.
Linsie aligundua mahusiano hayo baada ya mumewe, siku ya kuadhimisha miaka 24 ya ndoa yao, kwa bahati mbaya kumtumia meseji ya simu iliyokuwa iende kwa Tracie. Mwanzoni alikana na kudai kwamba alikuwa tu marafiki.
Linsie alilieleza gazeti la The Sun: "Yule mwanamke ameniibia mume wangu."
"Alinieleza wangekuwa na wazungumzo tu lakini anadai sasa ni mwanasaikolojia aliyepatiwa mafunzo na nafikiri amemtawala."
Wanandoa hao mwanzoni walijaribu kuzifanyia kazi tofauti zao lakini ndoa hiyo mwishowe ikasambaratika baada ya kishindo hicho cha mwisho.
Linsie aliondoka kwenye nyumba hiyo ya familia waliyokuwa wakiishi pamoja na mtoto wao wa kiume, Michael mwenye miaka 16, na binti yao Jordie mwenye miaka 20.
Kwa sasa anaishi kwenye ghorofa dogo na anadai talaka, lakini anasema anahofia kuhusu usalama wa mume wake.
Tracie mwanzoni alikana kumuua Lee, akidai aliuawa na dereva katika mbio za magari barabarani karibu naAlvechurch, Worcestershire. Kisha baadaye akadai alimuua katika harakati za kujilinda.
Phil, ambaye ana watoto wawili wenye umri wa kati ya miaka 30 na 31 katika mahusiano yake yaliyopita, alikanusha kuwa na mahusiano na muuaji huyo. Alilieleza gazeti la The Sun: "Hiyo si kweli."

No comments: