CHEKA TARATIBU...

Wakati mwingine wanawake wanawahisia vibaya waume zao kupita kiasi. Wakati Adam akichelewa kurudi kwa siku chache, Eva anakasirika sana. "Unakula raha na wanawake wengine mitaani," analalamika Eva.
Adam anajibu, "Umekosa cha kuongea we mwanamke. Wewe ni mwanamke pekee duniani." Mzozo uliendelea hadi Adam akapitiwa na usingizi ndipo aliposhituliwa pale alihisi mtu akimpapasa kifuani mwake.
Alikuwa Eva. Ndipo Adam akauliza, "Unafanya nini?"
Eva akajibu kwa upoole, "Nahesabu mbavu zako!" Kaazi kwelikweli...

No comments: