Washitakiwa wa kesi ya
mauaji ya mjumbe wa Tume ya Taifa ya Mabadiliko ya Katiba, Dk Sengondo Mvungi
wameiomba Mahakama iwape haki ya kuwasikiliza.
Waliwasilisha ombi hilo
jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi Waliarwande
Lema wakati kesi hiyo ilipotajwa na Wakili wa Serikali, Leonard Challo kudai
upelelezi bado haujakamilika.
Mshitakiwa Longishu
Losingo alidai wapo jela, lakini wanatakiwa kupata haki zao za msingi kwa
sababu wanaona Mahakama inaegemea upande mmoja, hoja zao hazisikilizwi.
Hakimu Lema alisema
hawezi kuwasikiliza na alishatoa kibali waende kwa Hakimu Mfawidhi wa Mahakama
hiyo. Aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 23, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.
Mbali na Longisho,
washitakiwa wengine ni Chibago Magozi (32), John Mayunga (56), Juma Kangungu
(29), Paulo Mdonondo (30), Mianda Mlewa (40) , Zacharia Msese (33) Msigwa
Matonya (30) na Ahmad Kitabu (30).
Wanadaiwa kuwa Novemba 3,
mwaka juzi katika eneo la Msakuzi, Kibwegere wilayani Kinondoni jijini Dar es
Salaam, walimuua Dk Mvungi kwa kukusudia.
No comments:
Post a Comment