Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es
Salaam, iliimarisha ulinzi wakati kesi ya ugaidi inayomkabili Kiongozi wa
Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (Jumiki), Shekhe Farid Hadi
Ahmed na wenzake ilipotajwa.
Askari walikuwa wengi katika eneo la Mahakama
huku kila mtu aliyeingia getini akikaguliwa
kwa kifaa maalumu na kupapaswa ili kuangalia kama ana silaha.
Jana kesi hiyo ilitajwa mbele ya Hakimu Mkazi
Janeth Kaluyenda na kuahirishwa hadi Machi 4 mwaka huu itakapotajwa tena.
Wakili wa Serikali, Peter Njike alidai kuwa
kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa lakini bado wanasubiri uamuzi wa rufaa
waliyoikata katika Mahakama ya Rufani.
Upande wa Jamhuri ulikata rufaa kupinga uamuzi
wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ulioamuru Mahakama ya Kisutu kusikiliza
na kutolea uamuzi hoja za washitakiwa.
Washitakiwa wanadaiwa kati ya Januari mwaka
jana na Juni mwaka huu katika maeneo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
walikula njama ya kutenda kosa kwa kutafuta watu wa kushiriki vitendo vya
ugaidi.
Katika mashitaka mengine, wote wanadaiwa
katika kipindi hicho, huku wakijua ni kosa walikubaliana kuwaingiza nchini,
Sadick Absaloum na Farah Omary washiriki vitendo vya ugaidi.
No comments:
Post a Comment