TRL YAKIRI TRENI YA ABIRIA DAR MBOVU


Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) imesema ubovu wa treni inayotoa huduma  ya usafiri wa abiria  katika jiji la Dar es Salaam unatokana na  kuzeeka kwa  injini jambo linalosababisha kuwepo kwa matatizo mbalimbali kama kuzima.

Msemaji wa TRL, Midladjy Maez alisema hayo ofisini kwake  wakati akizungumza na HabariLeo  kuhusu ubovu wa treni hiyo iliyozimika  ikitoa huduma na  kusababisha  usumbufu kwa abiria.
“Yapo mambo mengi ambayo siwezi kuyasema…uzee umeongezeka kwa injini hizo haswa ukikumbuka kuwa zilipoanza kazi hazikuwa mpya bali ni zilizoboreshwa …ilikuwa kama huduma ya reli yaanza kwa spana mkononi,” alisema Maez.
Alisema  kila wakati huduma hiyo imekuwa na matatizo yaliyokuwa yakihitaji marekebisho ya kiufundi  lakini kimsingi zinahitajika injini mpya za kisasa  na tayari maombi ya vifaa hivyo yalishawasilishwa serikalini tangu wakati wa Waziri aliyekuwapo  Dk  Harrison Mwakyembe.

No comments: