KESI YA KUMDHURU MFANYAKAZI WA NDANI YAPIGWA KALENDA


Kesi ya kumdhuru mfanyakazi wa ndani inayomkabili raia wa Ufaransa, Folkertsma Laurent (41), imeahirishwa hadi Machi 31, mwaka huu kutokana na shahidi kutofika mahakamani.

Awali, Wakili wa Serikali, Felista Mosha wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala, alidai kwamba kesi hiyo jana ilikuja kwa ajili ya kusikilizwa na kwamba shahidi waliyemtegemea mahakamani hapo hakufika.
Pia alidai kuwa shahidi huyo alipewa onyo afike mahakamani hapo ili kuendelea na ushahidi huo lakini hakufanya hivyo na kwamba hakutoa taarifa.
Hakimu Mkazi Mwandamizi, Juma Hassani aliahirisha kesi hiyo hadi Machi 31, mwaka huu upande wa Jamhuri utakapoendelea kusikiliza kesi hiyo.
Hata hivyo, mshitakiwa huyo alidai kuwa Wakili anayemuwakilisha alipatwa na msiba hivyo alisafiri lakini mpaka anafika mahakamani hakujua kama amesharudi au la.
Ilidaiwa  Mei 23, mwaka huu, maeneo ya Tabata Liwiti Wilaya ya Ilala, Laurent alimpiga na kumsukuma Aneth Mponzi na kumsababishia maumivu mwilini. Mshitakiwa yupo nje kwa dhamana.

No comments: