Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni ya Clouds Media Group, Joseph Kusaga amesema kuwa habari
zilizoenea mtaani kwamba kampuni hiyo imeuzwa ni za uzushi na kuwataka
Watanzania wazipuuze.
Kampuni
hiyo ambayo inamiliki Clouds FM, Clouds Tv na Choice FM ilidaiwa kuuzwa kwa
mmoja wa wafanyabiashara maarufu na kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Kusaga (pichani)
alisema habari hizo ambazo zilisambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii
zilisababisha usumbufu mkubwa kwa wafanyakazi na viongozi wa Clouds pamoja na Watanzania kwa ujumla.
Alisema
habari hiyo imetengenezwa na watu walioamua kupoteza muda wao katika mitandao
ya kijamii, lakini wapo wanaovuna fedha nyingi kwa kupitia njia hiyo ya
mawasiliano.
Alisema
mara baada ya kuenea kwa habari hiyo, usumbufu mkubwa uliibuka kutokana na watu
wenye mapenzi mema na kampuni hiyo kuanza kuhoji juu ya taarifa hizo kama zina
ukweli.
“Clouds Media Group ni kampuni iliyoanzia chini kwa ushirikiano wa watu wengi, hivyo kuamua kuiuza kiholela ni jambo la kushangaza, ingawa pia si dhambi kufanya hivyo kwa mtu yoyote kwa sababu ni biashara kama zilivyokuwa biashara nyinginge," alisema.
Aidha Kusaga aliwahakikishia Watanzania kuwa Clouds ni chombo huru kisichofungamana na chama chochote cha siasa, huku akisema kwamba katika Uchaguzi Mkuu mwaka huu haki itatolewa kwa vyama vyote na wanasiasa wote.
“Huu ni mwaka mgumu, hivyo naomba niseme ikitokea suala la kuhoji au kuunga mkono siasa, basi haki itatolewa kwa wanasiasa wote, ukizingatia kwamba chombo chetu hakika chama cha siasa inachokiunga mkono kwa sababu zozote zile,” alisema Kusaga.
“Clouds Media Group ni kampuni iliyoanzia chini kwa ushirikiano wa watu wengi, hivyo kuamua kuiuza kiholela ni jambo la kushangaza, ingawa pia si dhambi kufanya hivyo kwa mtu yoyote kwa sababu ni biashara kama zilivyokuwa biashara nyinginge," alisema.
Aidha Kusaga aliwahakikishia Watanzania kuwa Clouds ni chombo huru kisichofungamana na chama chochote cha siasa, huku akisema kwamba katika Uchaguzi Mkuu mwaka huu haki itatolewa kwa vyama vyote na wanasiasa wote.
“Huu ni mwaka mgumu, hivyo naomba niseme ikitokea suala la kuhoji au kuunga mkono siasa, basi haki itatolewa kwa wanasiasa wote, ukizingatia kwamba chombo chetu hakika chama cha siasa inachokiunga mkono kwa sababu zozote zile,” alisema Kusaga.
No comments:
Post a Comment