Hospitali
26 za rufaa katika mikoa 25 nchini, zitafanyiwa
maboresho ili zitoe huduma bora za afya kupitia mradi wa Japan
International Co-operative Agency (JICA) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya na
Ustawi wa Jamii.
Akizungumza
katika mkutano wa tathimini ya miradi mingine ya afya iliyotekelezwa, mwakilishi wa shirika la Jica, Kuniaki Amatsu
alisema mpango huo umeonesha ufanisi mkubwa katika utekelezaji wake na
kuwezesha wananchi kupata huduma bora za afya.
“Uboreshaji
wa huduma za afya umekuwa na matokeo mazuri na tumeshuhudia mabadiliko katika
hospitali nyingi, ikilinganishwa na hali ilivyokuwa hapo awali. Mazingira
yamekuwa mazuri na utaratibu mzuri wa mpangilio wa utoaji huduma,” alisema
Amatsu.
Akizungumzia
hali ilivyokuwa katika hospitali nyingi za rufaa kabla ya kuanza kwa
utekelezaji wa uboreshaji huduma mwaka 2011, alisema kwa sasa mandhari za
hospitali ni nzuri na mazingira pia yanafurahisha katika upatikanaji wa huduma
za afya.
“Hospitali
zimekuwa na mandhari nzuri na hata ufanisi wa utoaji huduma pia umeongezeka
ikilinganisha na kipindi cha nyuma kabla mradi huu haujaanza kutekelezwa katika
hospitali hizo,” alisema.
Hospitali
zilizoonesha mafanikio ambazo zitaanza kutekelezewa maboresho mengine ambayo
mafanikio yake yatatumika katika maboresho ya sekta ya afya Afrika ni pamoja na
Mawenzi (Kilimanjaro), Bukoba (Kagera), Mbeya (Mbeya), Morogoro (Morogoro),
Shinyanga (Shinyanga).
Nyingine
ni Bombo (Tanga), Songea (Songea), Musoma (Mara), Maweni (Kigoma), Iringa
(Iringa), Sokoine (Lindi), Amana, Mwananyamala na Temeke za Dar es Salaam,
Ligua (Mtwara), Tumbi (Pwani), Sekou-Toure (Mwanza), Dodoma (Dodoma), Mount
Meru (Arusha), Singida (Singida), Kitete (Tabora), Sumbawanga (Rukwa), Bariadi
(Simiyu), Mpanda (Katavi), Geita (Geita), Kibena (Njombe), na Manyara
(Manyara).
Akizungumzia
mradi huo mpya wa uboreshaji hospitali za rufaa za mikoa utakaoanza mwezi ujao,
Amatsu alisema wanahitaji kuongezea ufanisi katika utoaji wa huduma, ikiwa ni
pamoja na kuwezesha watoa huduma kupata mafunzo bora ya kutoa huduma.
Watoa
huduma hao pia watafundisha namna na umuhimu wa utunzaji wa kumbukumbu za
kitabibu, jinsi ya kuweka mipangilio mizuri ya vifaa tiba na dawa katika
mazingira ya hospitali na kutunza mazingira ya hospitali.
“Mradi
mkubwa unaotarajia kuanza mwezi ujao, utajumuisha hospitali za rufaa zipatazo
ishirini na sita zitakazoboreshwa kwa kupatia mafunzo madaktari na watoa huduma
wengine, ili kuwa na ufanisi mzuri wa kutoa huduma za afya.
“Hospitali
hizo zitapatiwa vifaa tiba kwa ajili ya kuongeza ufanisi wa matibabu, kuwezesha
hospitali kutatua matatizo madogo bila kuhitaji msaada wa nje na kufundisha
watoa huduma jinsi ya kutunza kumbukumbu za matibabu na takwimu nyingine za
kitabibu,” alisema Amatsu.
Akifungua
mkutano huo, Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa
Jamii, Bernard Kongo, aliishukuru
Serikali ya Japan kwa kuendelea kusaidia Tanzania kuboresha huduma za
afya, kwani kupitia shirika la Jica hospitali nyingi zimeboreshwa na kuwa na
uwezo mkubwa wa utoaji wa huduma za afya.
Aliongeza,
“mradi huu utakaoanza, utasaidia kwa kiasi kikubwa katika upanuzi wa huduma za
afya hapa nchini. Hospitali zetu za rufaa zitatoa huduma za haraka na zenye
ufanisi mkubwa ikilinganishwa na hapo awali,” alisema Kongo.
Akizungumzia
jinsi walivyonufaika na mradi huu, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dk Archie
Hellar, alisema hospitali za mkoa wake zimekuwa bora zaidi kwa kila kitu
ukilinganisha na hapo zamani.
No comments:
Post a Comment