BUNGE LAPATA WENYEVITI WAPYA

Bunge  la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, limepata wenyeviti  wapya wawili wa Bunge watakaosaidia na Spika na Naibu Spika kuongoza vikao vya Bunge ambao ni Mbunge wa Viti Maalumu, Lediana Mng’ong’o (CCM) na Mbunge wa Viti Maalumu, Kidawa Hamis Saleh (CCM).

Mng’ong’o anachukua nafasi ya mbunge wa Peramiho, Jenista Mhagama (CCM) aliyeteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi na baadaye kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge).
Huku Saleh akichukua nafasi ya Mbunge wa Jimbo la Uzini, Mohammed Seif Khatib (CCM) kwa upande wa Zanzibar aliyeacha uenyekiti kwa sababu ambazo hazijafahamika.
Spika wa Bunge, Anne Makinda akihitimisha kikao cha Bunge juzi jioni, alisema kamati ya uongozi ilipendekeza majina hayo mawili kuziba nafasi hiyo na kwa mujibu wa kanuni za bunge yakiwa majina mawili ambayo yalipitishwa na wabunge wote.

No comments: