PROF. MBWETTE RAIS WA CHUO KIKUU CHA AFRIKA


Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Profesa Tolly Mbwette amechaguliwa kuwa Rais wa Baraza la Chuo Kikuu cha Afrika (Pan African University).

Atakuwa madarakani kwa miaka mitatu kuanzia juzi aliposhinda katika uchaguzi uliofanyika jijini hapa.
Aidha, Ekwabi Mujungu amechaguliwa kuwa Mjumbe wa Bodi ya Umoja wa Afrika inayoshughulika na mapambano dhidi ya rushwa kwa kipindi cha miaka miwili ijayo.
Uteuzi wao unatarajiwa kuthibitishwa na Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) utakaofanyika kwa siku mbili kuanzia leo jijini hapa.
Katika mkutano huo, Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa miongoni mwa marais na wakuu wa nchi  watakaoshiriki.
Serikali kupitia Ubalozi wake wa Addis Ababa chini ya Balozi Naimi Azizi, ulipiga kampeni kuhakikisha kuwa wagombea hao wanashinda nafasi hizo.

No comments: