Wakazi
wa vitongoji 11 katika vijiji vitatu
vya halmashauri ya wilaya ya Kilombero
mkoani Morogoro, wameshindwa kupiga kura kuchagua viongozi wa serikali za
vitongoji na vijiji, kutokana nna migogoro ya ardhi iliyopo kwenye vitongoji
hivyo.
Mkurugenzi
Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kilombero, Azimina Mbilinyi, alisema hayo
hivi karibuni mjini hapa.
Mbilinyi alisema tayari mgogoro hiyo ya ardhi,
mashauri yake yamefikishwa katika Mahakama Kuu ya Ardhi.
Alitaja
vitongoji hivyo kuwa ni vya kijiji cha
Chiwachiwa Kata ya Mbingu, Miomboni Kata ya Mofu na Idandu kilichopo
Kata ya Namawala.
Alisema
katika matokeo ya uchaguzi uliofanyika Desemba 14, mwaka huu, CCM wilaya ya
Kilombero imeshinda katika viti vya
vijiji 59 sawa na asilimia 55.1, Chama
cha Demorasia na Maendeleo (CHADEMA )
viti 39 sawa na 33.6, Chama cha Wananchi (CUF) vijiji 12 sawa na
asilimia 11.2 na NCCR-Mageuzi hakijashinda hata kiti kimoja.
Kwa
upande wa vitongoji , CCM kimepata viti 245 sawa na asilimia 50.6, CHADEMA viti 190 sawa na asilimia 39.3, CUF
viti 48 sawa na asilimia 9.92 na NCCR kiti kimoja sawa na asilimia mbili.
Watu waliojiandikisha kupiga kura walikuwa ni 143,058
na waliopiga kura walikuwa ni 116,485.
No comments:
Post a Comment