TRL YAKOPESHWA SHILINGI BILIONI 12


Kampuni ya Reli ya Kati (TRL) imepata mkopo wa Sh bilioni 12 kutoka Benki ya Maendeleo (TIB) kwa ajili ya kuongeza mtaji wa uendeshaji.
Makabidhiano ya mkopo huo yalifanyika  jana kati ya Mkurugenzi Mtendaji wa TIB,  Peter Noni na Mwenyekiti wa Bodi wa TRL, Severine Kaombwe.
 “Sisi kama TIB lazima tushiriki katika uwekezaji katika maeneo mbalimbali hapa nchini ila sasa tumeamua kuwasaidia TRL,” alisema Noni.
Mwenyekiti wa Bodi TRL, Kaombwe  alisema mtaji huo utawasaidia kufanya kazi bila tatizo. Alisema sasa wana vichwa sita ambavyo ni vizima na vinafanya kazi na wanategemea kupata vichwa vingine viwili.
 “Reli ni muhimu sana na ni mahali ambapo serikali inapenda kuwekeza hivyo kwa mtaji huu mambo yataenda vizuri,” alisema Kaombwe.

No comments: