TANGA YATAJA VITUO VITATU VYA KUDHIBITI EBOLA



Mkoa wa Tanga umetenga vituo kadhaa vya afya vitatu, ikiwa ni hatua ya maandalizi ya kudhibiti watu watakaobainika kuambukizwa virusi vya homa ya ebola.
Vituo hivyo ni cha kwenye mpaka wa Horohoro wilayani Mkinga, Masiwani Shamba na Maramba.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa alibainisha hayo juzi katika mkutano na waandishi wa habari.
Alisema timu maalumu ya mkoa ya wataalamu wa afya, tayari inakagua uwezo wa vituo vingine vilivyotengwa na halmashauri nyingine za mkoa huo, kama vinastahili kupokea wagonjwa wa aina hiyo.
Alisema ingawa mpaka sasa hakuna mgonjwa wa ebola nchini, serikali imechukua hadhari hiyo, kuwaondoa wasiwasi wananchi kutokana na mwingiliano wa wageni kutoka nchi jirani kupitia mpaka wa Horohoro.
Alisema vituo hivyo vitatu vimeimarishwa kwa kupelekewa vifaa tiba, madaktari na wauguzi wenye stadi za kutosha na vitatumika kutoa huduma kwa wagonjwa watakaobainika.
Kwa kuwa ebola haina chanjo wala tiba, mpango mkakati wa mkoa sasa ni kuhakikisha wananchi wanaelimishwa kuhusu namna ya kujikinga  kuzuia maambikizipia tumeziagiza halmashauri zote 11 zinazounda mkoa kutenga maeneo sahihi ya kupokelea wagonjwa hao, alisema.
Aliongeza, wananchi ondoeni wasiwasi na tunawataka muimarishe usafi wa mazingira, hakikisheni mnanawa vizuri mikono kwa maji safi na sabuniacheni kusalimia kwa kushikana mikono na watu kila mahali, alisema.

No comments: