Wasamaria wakihangaika kunasua majeruhi na miili ya marehemu kutoka kwenye basi la Morobest lenye namba za usajili T 258 AHV lililogongana uso kwa uso na lori lenye namba T 820 CKU kwenye eneo la Pandambili, mkoani Dodoma mapema leo majira ya Saa 2 asubuhi. Watu 17 wamethibitishwa kufariki na wengine zaidi ya 56 kujeruhiwa vibaya.

No comments: