Naibu
Waziri wa Viwanda na Biashara, Janeth Mbene amesema ipo haja ya pombe
zinazouzwa zikiwa zimefungwa kwenye mifuko midogo ya plastiki maarufu kama
viroba kuondolewa kwani ni janga la taifa linalosababisa ulevi kila eneo.
Waziri
huyo aliongeza kuwa pombe hizo zinauzwa
kiholela hadi katika mageti ya shule,
vibanda vya simu, barabarani, maduka ya bidhaa za vyakula na hata kwa akina mama ntilie.
Alisema
pombe hiyo imekuwa ikiuzwa bila usimamizi, jambo ambalo linatishia Taifa kuwa
la walevi na kuzitaka Manispaa kuangalia suala hilo kwani limekuwa tatizo kubwa.
Naibu
waziri huyo alisema kutokana na pombe hiyo kutowaletea tija watumiaji, pamoja
na kuwa na athari za mazingira ifikie
mahali mapendekezo yatolewe ili viondolewe katika soko na kuwa katika mfumo wa
chupa badala ya makaratasi.
Alisema
mbali na pombe hizo ambazo zipo zinazozalishwa nchini, lakini zipo ambazo
huingizwa kutoka nje ya nchi ambazo zinadaiwa kusababisha athari kwa watumiaji
kupata majipu katika fizi.
"Ebu
angalieni hili suala jamani, hivi viroba vimetapakaa kila mahali hata katika
maduka yanayouza chakula ni kwanini yanaruhusiwa kuuuza bidhaa hiyo,"
alisema Naibu Waziri.
Alisema
mbali na viroba hivyo kusababisha madhara ya kiafya lakini pia zinachafua
mazingira kwani makaratasi yanayohifadhia hutupwa na kuzagaa ovyo mitaani.
Akizungumza,
Mwakilishi kutoka Manispaa, Jumanne Ndaigeze alisema ni vyema tatizo hilo
likajadiliwa na mapendekezo kutolewa ili pombe hiyo iondolewe na kuwekwa kwenye
chupa ili kuondokana na makaratasi.
"Kwa
kweli kama hali kama ndivyo ilivyo basi ifikie mahali kweli yawepo majadiliano
ili pombe hiyo iweze kuondolewa," alisema Ndaigeze.
No comments:
Post a Comment