Hali
si shwari katika sekta ya elimu katika wilaya za Kalambo na Sumbawanga mkoani Rukwa, baada ya kuelezwa idadi kubwa
ya wanafunzi wa kiume katika shule za sekondari hukatisha masomo ili kujikita
katika kutunza familia, kwani wengi wao ni waume za watu, wengine wakiwa na wake
hadi watatu.
Kwa
kiasi kikubwa, dhana iliyopo ni kwamba wanawake ndio wanaokatishwa masomo
kutokana na sababu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kupata ujauzito au
kulazimishwa kuolewa katika umri mdogo.
Hayo
yalibainika katika kikao
cha siku moja cha Wadau wa Elimu
kilichowakutanisha Waratibu Elimu Kata, Maofisa Elimu wa Wilaya
za Kalambo na Sumbawanga na
kufanyika juzi mjini hapa nchini ya uratibu wa Asasi isiyo ya Kiserikali ya TMEP
kupitia mradi wake
wa afya ya uzazi na ujinsia unaotekelezwa mkoani Rukwa
na taasisi isiyo ya Kiserikali ya Resource Oriented Development Initiative (RODI).
Mkuu wa Shule
ya Sekondari Kasanga iliyopo
katika mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Kalambo, Christopher Sinyangwe ndiye aliyeibua hoja, baada ya kueleza kuwa
utoro sugu ni changamoto kubwa katika
shule hiyo, akisema kati ya
wanafunzi 80 wanaoanza kidato cha kwanza, mara nyingi wanaohitimu hawazidi 30.
Aliongeza
kuwa sababu kubwa
ni mwamko mdogo wa elimu
kwa upande wa wazazi na
walezi ambao wanawaozesha
watoto wao mara
tu wanapoingia Kidato cha Kwanza
na kuwaacha wake zao katika
vijiji wanavyotoka hivyo wanalazimika
mara kwa mara kukatiza
masomo yao ili
waweze kurudi nyumbani kuwajibika
kwa familia zao.
"Zipo taarifa
za uhakika kuwa wanafunzi
wa kiume kuwa na wake wawili hadi
watatuÉbaadhi yao wanaanza Kidato cha Kwanza tayari
wameshaoa, wakifika Kidato cha
Tatu tayari ana wake
watatu au wawili na watoto ambao
anawajibika kuwahudumia hivyo
wanakatiza masomo na kujihusisha
na shughuli za uvuvi
kwa muda ili kuzikimu familia
zao kisha hurejea shuleni," aliongeza Sinyangwe.
Kwa
mujibu wa Kaimu Ofisa Elimu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo, Japhet Buchwa ambaye
pia ni Ofisa Elimu Taaluma (Sekondari) alibainisha kuwa utoro
sugu ni changamoto
kubwa shuleni kwa
upande shule za
umma watoto 600 walikatiza masomo
yao kwa kipindi cha
Januari hadi Februari mwaka
huu.
Alisema
katika kipindi hicho cha kati ya
Januari na Februari mwaka huu
wanafunzi wapatao 23 kutoka
shule za sekondari za binafsi
wamekatiza masomo yao
kwa sababu mbalimbali zikiwemo
za ujauzito.
Kwa
mujibu wa Buchwa, watoto wapatao 4,913
wanasoma katika shule
za sekondari za umma wilayani humo
ambapo shule za sekondari za
binafsi zina wanafunzi wapatao 300.
Akichangia uzoefu
wake, Mratibu Elimu Kata ya
Mfinga katika Bonde la Ziwa Rukwa wilayani Sumbawanga alibainisha kuwa kutokana na
mwamko duni wa elimu wazazi
huwaozesha watoto wao wa kike kwa mahari kati
ya ng'ombe 25 hadi 30
pia kwa watoto
wa kiume wanarubuniwa na wazazi wao
kukatiza masomo yao na kuwaajiriwa kama
vibarua mashambani na kuchunga
mifugo.
"Wengi wa wazazi
na walezi ambao hawaoni
umuhimu wa elimu
wanadai ni bora watoto
wao wakaoe au kuolewa
kuliko kuendelea na masomo isitoshe baadhi
ya wazazi huwatishia maisha walimu wanapofuatilia
watoro sugu," alibainisha.
Naye
Mratibu Elimu Kata ya Mpui wilayani Sumbawanga, Tabia Mkembo
alibainisha kuwa kutokana
na Shule ya Sekondari Mpui kutokuwa na
uzio, wanafunzi wa kike wanadaiwa
kutoroka usiku na kwenda kufanya ufuska hivyo baadhi yao
kupata ujauzito maarufu kama 'mimba
za minadani'.
Alidai
vibarua wa kampuni ya
ujenzi inayojenga barabara
ya Laela -Ð Sumbawanga kwa
kiwango cha lami
ni miongoni mwa watuhumiwa wa 'kuoa'
watoto wa kike shuleni hapo
ambapo baadhi ya wasichana wanaoishi
katika hosteli shuleni hapo wanashawishika kutoroka
usiku na kwenda
kwa 'waume' zao hao kutokana na
shule hiyo kutokuwa na uzio.
"Tuna taarifa kuwepo kwa visa
kwa wasichana wanaoishi
katika mabweni shuleni
hapo kutoroka
na kwenda kulala katika bweni
la wavulana Hapa walezi
wa watoto hawa 'patroni ' na 'matroni' wanapaswa kuwafuatilia kwa
karibu watoto hawa," alisisitiza.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa RODI, Gideon Mpina alizitaka
Halmashauri kuunda sheria ndogo
ndogo zitakazo zipa nguvu
za kisheria mamlaka husika kuwasaka wazazi na
walezi wote watakaobainika kuwaozesha watoto wao
wanaosoma ili sheria
iweze kuchukua mkondo
wake
No comments:
Post a Comment