Asilimia
kubwa ya watanzania waliohojiwa na taasisi ya utafiti wamesema mapato
yatakayopatikana kutokana na gesi yatumike katika huduma za afya na elimu.
Hayo
yalisemwa jana, Dar es Salaam na Mtafiti wa Taasisi ya Twaweza, Elvis Mushi
wakati akiwasilisha utafiti walioufanya wakishirikiana na Benki ya Dunia.
Alisema
Watanzania asilimia 43 wangependa mapato yote yaende serikalini kwa ajili ya
kugharamia huduma muhimu zikiwemo za afya na elimu. Alisema wananchi wanne kati
ya 10 waliohojiwa katika utafiti huo walipendekeza yatumike katika miundombinu
na kupambana na umasikini.
Mushi
alisema zaidi ya nusu ya Watanzania ikiwa ni sawa na asilimia 55 wangependa
baadhi ya mapato ya mafuta na gesi wapewe wananchi moja kwa moja kwa fedha
taslimu.
“Ili
kuleta maendeleo kuna asilimia 17 ya wananchi wangependelea serikali ipate
asilimia kubwa zaidi ya mapato kwa ajili ya kuendeleza miundombinu na huduma za
kijamii na wananchi wagawiwe kiasi kinachobaki,” alisema Mushi.
Alisema
ingawa makadirio ya sasa yanaonesha uchimbaji mkubwa wa mafuta na gesi huleta
faida katika kipindi cha miaka saba hadi kumi ijayo, wananchi asilimia 36
wanaamini kuwa makampuni ya gesi tayari yanapata fedha kutokana na ugunduzi
huo.
No comments:
Post a Comment