Wizara
ya Uchukuzi imesaini mkataba na Uholanzi kwa ajili ya kuongeza wigo wa safari
za ndege baina ya nchi hizo (BASA)
kukabili changamoto za usafiri wa anga
pamoja na kuongeza ulinzi na usalama wa anga.
Mkataba
huo ulisainiwa jana Dare s Salaam kati
ya Waziri wa wizara hiyo, Dk Harrison Mwakyembe na Balozi wa Uholanzi
nchini, Jaap Frederiks.
Akizungumza baada ya kutia saini mkataba huo, Dk
Mwakyembe alisema makubaliano hayo
yataweza kutoa fursa nzuri kwa
wasafiri wa nchi hizo pamoja na mizigo.
Alisema
hiyo ni fursa kwa mashirika mengine kati ya nchi hizo kujitokeza na kutoa huduma
kwa kuongeza idadi ya safari. Pia kutakuwa na ushindani wa nauli pamoja na kuongeza vituo na kulinda haki za abiria.
Kwa
mujibu wa Waziri, ndege zinazofanya safari katika nchi hizo zitatua katika viwanja vya Songwe na Mwanza tofauti
na awali ambapo walitumia vituo vya Zanzibar, Uwanja wa Kimataifa wa Julius
Nyerere (Dar es Salaam) na Mwanza.
Dk
Mwakyembe alisema awali makubaliano kama
hayo yaliwahi kufanyika mwaka 1978 ambapo masuala ya anga yalikuwa na upeo
mdogo.
Balozi Jaap alisema soko la Tanzania limekuwa
likikua, ikiwa ni pamoja na sekta ya usafiri ambalo ni eneo maalum la kukuza
utalii na biashara.
No comments:
Post a Comment