Wizara
ya Katiba na Sheria imeanza kuboresha kazi ya kusajili vizazi kwa kugatua
majukumu hayo kutoka serikali kuu kwenda serikali za mitaa.
Mkakati
huo tayari umeanza kutekelezwa katika wilaya ya Temeke mkoani Dar
es Salaam na halmashauri zote za mkoa wa Mbeya.
Pia,
Wizara hiyo imetangaza kuwa inatarajia kuboresha usajili wa vizazi hadi kufikia asilimia 20 mwakani kutoka
asilimia 6.5 za sasa.
Aidha
Wizara hiyo imefafanua gharama ambazo Mtanzania, anapaswa kulipa pale
anapohitaji cheti cha kuzaliwa, ambapo mtoto au mwombaji ambaye ameandikishwa
ndani ya siku 90 tangu azaliwe, gharama ya cheti hicho ni Sh 3,500 tu.
Kwa
mtoto au mwombaji ambaye alichelewa kuandikishwa, yaani baada ya siku 90 tangu
azaliwe lakini chini ya miaka 10, gharama ni Sh 4,000; na kwa usajili ya
mwombaji aliye na umri zaidi ya miaka 10 tangu kuzaliwa gharama ni Sh 10,000.
Naibu
Waziri wa Katiba na Sheria, Angella Kairuki alisema hayo alipojibu swali la
Mbunge wa Viti Maalum, Pauline Gekul (Chadema). Gekul aliuliza “ Je, ni gharama
kiasi gani anapaswa kulipa Mtranzania pale anapohitaji cheti cha kuzaliwa?”
Kairuki
alisema cheti cha kuzaliwa hutolewa chini ya Sheria ya Uandikishaji wa Vizazi
na Vifo Sura ya 108. Sheria hiyo kupitia Tangazo la Serikali Namba 245 la Julai
2000 imeainisha gharama za uandikishaji na utoaji wa cheti cha kuzaliwa.
Gharama hizo zinatofautiana kutokana na aina ya kizazi
kinachohitaji
kusajiliwa na muda wa kusajili kizazi.
Alisema
Wakala wa Usajili, Udhamini na Ufilisi (RITA) umeendelea kuboresha mfumo wa
usajili wa vizazi kupitia Mkakati wa Usajili wa Watoto walio chini ya Miaka
Mitano (U5BRI) kwa awamu.
“Kupitia
mkakati huo serikali imeomdoa gharama ya ada ya cheti kwa toleo la kwanza kwa
watoto wenye umri huo kwenye maeneo ambayo mkakati huu umeanza kutekelezwa
hususan wilaya ya Temeke na katika halmashauri zote za mkoa wa Mbeya.
Halmashauri za mkoa wa Mbeya ni Mbeya, Mbarali, Chunya, Mbozi, Momba, Rungwe,
Ileje na Kyela na Halmashauri ya Jiji la
Mbeya.
No comments:
Post a Comment