Wabunge
wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) wamesisitiza kuwa mpango wa kumng’oa Spika wa Bunge hilo, Margaret Zziwa
liko pale pale licha ya wabunge watatu wa Tanzania kuondoa saini zao.
Baada
ya Zziwa kumaliza kusoma sala na kukaribisha kusomwa kwa bajeti, hatua hiyo
haikufanyika kwani baadhi ya wabunge walianza kupiga kelele kulalamika kuwa
hakuna ajenda ya kung’olewa kwa spika kwenye shughuli za siku hiyo.
Mbunge
Shyrose Bhanji alisimama na kusema
wabunge wa Tanzania akiwemo, Adam Kimbisa, na Mariamu
Ussi wameondoa saini zao katika azimio la kuunga mkono kung’olewa kwa Spika
Zziwa madarakani.
Alisema
ni kweli Zziwa ana upungufu wake lakini mchakato wa kumwondoa madarakani
una hatua zake moja baada ya nyingine. Alisema, “sasa nimegundua kuna ajenda ya
siri ambayo imezidi yale mapungufu ya spika na ndiyo lengo la kutaka kumuondoa
madarakani.”
Bhanji
alisema amejaribu kuelewesha kwamba kama
wabunge hao wanataka kwenda na jambo hili si vibaya wakienda nalo hatua kwa
hatua ingawa baadhi yao, wanataka lichukuliwe bila utaratibu.
Alisema
bunge hilo lilikuwa linatakiwa kusoma Bajeti ya Afrika Mashariki tangu juzi
lakini mpaka sasa hivi wabunge wamekataa badala yake, wanataka suala la
kung’olewaa spika ndio lipewe kipaumbele.
Aliendelea
kusema, “Na utaratibu wa kumuondoa Spika unasema lazima kuwe na saini za
wabunge wanne kutoka kila nchi wanachama na kwa sababu hiyo Tanzania saini
zimebakia mbili, basi kwa sasa azimio hili limeshakufa halina nguvu tena
kisheria.”
“Nimeliangalia suala hili kwa mapana yake na
kuona masuala ya wananchi wa Afrika Mashariki ndio jambo muhimu linalopaswa
kupewa kipaumblele na si ajenda hii ambayo pengine kuna ajenda iliyojificha
nyuma yake”, alifafanua Bhanji.
Mwanasheria
wa EAC na Bunge hilo, Wilbert Kahwa
alisema kutolewa kwa saini za wabunge watatu wa Tanzania haina maana kwa sababu
saini hizo zilikuwa ni kwa ajili ya kuunga mkono jambo hilo katika hatua za
awali kwa ajili ya kutengeneza azimio, sasa azimio tayari
limeshatengenezwa na lipo ndani ya
Bunge.
“Saini hizo 3 haziwezi kuzuia azimio la
kumng'oa Spika kwani tayari ilishafika bungeni azimio linaenda mbele halirudi
nyuma,” alisema.
Awali
wabunge hao kutoka nchi za EAC walikuwa na malalamiko ya kutokuwa na imani na
Zziwa na kuazimia kumng'oa. Baadhi ya wabunge wanajitoa katika msimamo huo ili bajeti ya EAC iweze
kupitishwa.
No comments:
Post a Comment