Mji wa Sumbawanga mkoani Rukwa umetajwa kuwa unaelemewa na idadi kubwa
ya watoto wa mitaani
wanaorandaranda katika kona ya
mji huo, huku baadhi
yao wakidaiwa kutumika
na makundi ya kihalifu.
Wengi
wa wadau wameingiwa
na hofu kutokana na idadi kubwa
ya watoto hao wenye umri wa
miaka kati ya miaka 3-15, wakidai ni 'bomu' tarajiwa
iwapo mamlaka husika
hazitakuwa na mikakati
dhabiti ya kupambana na
tatizo hilo.
Kwa mujibu wa Ofisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya
Sumbawanga, James Biseko, manispaa hiyo ina idadi ya watoto 7,870 wakiwemo watoto
wanaishi katika mazingira
magumu na wale
wanaoishi mitaani mjini
Sumbawanga.
Hata
hivyo, kutokana na idadi
kubwa ya watoto wanaoishi mtaani
Mjini Sumbawanga, ofisa huyo amekiri
kuwa hana takwimu rasmi
ya watoto hao.
Uchunguzi uliofanywa
na mwandishi wa habari
hizi umebaini kuwa watoto hao
wanaoishi mitaani mjini hapa wanaishi katika
vikundi wakiwa na uongozi wao
ambapo wale wenye umri mdogo
ndio 'wahasibu' wa
vikundi hivyo.
Wamekiri baadhi yao kutumiwa na makundi ya kihalifu
hususani wale wenye maumbile
madogo ambapo wanapitishwa
madirishani usiku wakielekezwa
wakiingia ndani wafungue
milango ya nyumba kisha 'wahalifu' hao
huingia ndani na kuiba .
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda amekiri kuwa
watoto wa mitaani ni tatizo
ambalo linaongezeka kila kukicha.
No comments:
Post a Comment