Mkoa wa Tabora unaongoza kwa mauaji ya
wanawake na vikongwe kunakotokana na kukithiri kwa imani za kishirikina.
Hayo yamesemwa na Kamishna wa polisi
jamii nchini, Mussa Ally Mussa akiwa katika kijiji cha Idudumo kata ya Miguwa
wilayani Nzega kuwa mkoa wa Tabora unaongoza kwa mauaji ya wanawake kwa sababu
mbalimbali ikiwepo za ushirikina.
Mussa akizungumza na jeshi la jadi la
sungusungu alisema kuwa mkoa huo wa Tabora unapaswa kubadilika na kuachana na
mauaji ya wanawake na vikongwe na tayari jeshi hilo la jadi kwa kushirikiana na
polisi wamedhibiti mauaji hayo.
Alisema sababu za kuuawa kwa wanawake
ni sababu ambazo si za msingi kwa jamiii na badala yake husababisha yatima
ikiwa na kukatisha maisha ya watu.
Mussa alisema sungusungu wanapaswa
kushirikiana na jeshi la polisi kwa nyakati mbalimbali ili kuhakikisha wahalifu
wanakosa nafasi katika kufanya uhalifu huo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Suzan
Kaganda alitoa filimbi 12 zitakazosaidia kuimarisha ulinzi katika kijiji hicho.
No comments:
Post a Comment