Mamlaka
ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) imesisitiza kwamba,
mabasi ya Shirika la Usafirishaji Dar es Salaam (UDA) yanatakiwa kupaka rangi
kulingana na njia na si kuweka vibao pekee.
Meneja
Mawasiliano wa Sumatra, David Mziray alikiri mamlaka yake, wiki iliyopita,
ilitoa agizo kwa Uda kuhakikisha mabasi yake yanapakwa rangi kama ilivyo
kwa daladala za kawaida na kuweka vibao kuonesha njia wanakotoa
huduma.
Hata
hivyo alisema mpaka sasa, shirika hilo halijatekeleza agizo hilo hali ambayo
imelazimu mamlaka kukamata mabasi matano kutokana na kukiuka masharti
hayo.
Mziray
alisema kama hawatatekeleza, mamlaka itaendelea kuwakamata.
“Makubaliano
tuliyofanya na Uda ni kupaka rangi na kuweka vibao na si vibao pekee kama Uda
wanavyodai,” alisema Mziray.
Alisisitiza,
“Sisi tutaendelea kukamata magari yao kama hawatatekeleza agizo hivyo ni vizuri
wakubaliane ili kuondoa usumbufu.”
Hayo
yamekuja baada ya Uda kutoa taarifa kuwa wamekubaliana na Sumatra kuweka vibao
na si rangi kitendo amacho Sumatra wamepinga.
Akizungumza
hivi karibuni na mwandishi, Mkuu wa UDA, Hamdy Al Hadj alisema makubaliano yao
na Sumatra ni kuwepo kwa vibao katika magari yao kuonesha njia wanazotoa
huduma na si kupaka rangi.
“Kwa mfano kama basi linakwenda Gongo la Mboto
basi katika kibao kilichoko mbele ya basi kiwe na rangi ya eneo hilo kama
ilivyo katika daladala,” alisema Hamdy.
Alisema
tayari Shirika hilo linaendelea kukamilisha uwekwaji wa vibao hivyo mbele ya
mabasi yote yanayotoa huduma pamoja na kwamba nyuma ya mabasi kumewekwa namba
ili abiria waweze kutoa taarifa pindi watakapohudumiwa tofauti.
No comments:
Post a Comment