Mlima Kilimanjaro umepoteza takribani
asilimia 30 ya theluji kuanzia mwaka 1912 mpaka sasa, Bunge limeelezwa.
Naibu
Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Ummy Mwalimu, alisema
kuyeyuka kwa theluji katika kilele cha mlima huo kumechangiwa na mabadiliko ya
tabia nchi.
Mwalimu
alifafanua kwa kuzingatia utafiti ulifanywa na Taasisi ijulikanayo kama
Intergovernmental Panel on Climate Change (IPCC).
Alikuwa
akijibu swali la Mbunge wa Ole, Rajabu Mbarouk Mohamed (CUF) aliyetaka kujua
juhudi zilizofanywa na serikali kulinda mlima na wananchi wa vijiji vya
karibu.
Pia
alitaka kujua ni kiasi gani cha theluji kilichopungua kutokana na athari ya
mabadiliko ya tabia nchi.
Mwalimu
alitaja baadhi ya juhudi za serikali na jumuia za kimataifa kuwa ni pamoja na
kukabiliana na uharibifu unaochangiwa na mabadiliko ya tabia nchi kwa asilimia
5.3 kulingana na Mkataba wa Itifaki ya Kyoto na wa Umoja wa Mataifa (UNFCCC).
Alisema
Mkoa wa Kilimanjaro unatekeleza progamu ya maendeleo endelevu ya matumizi ya
ardhi katika kuzingatia mabadiliko ya tabia nchi, mpango ambao pia unatekelezwa
katika nchi za Afrika.
Alisema
mpango huo wa miaka minne (2011-2015) umefadhiriwa na Mfuko wa Maendeleo wa
Umoja wa Mataifa (UNDP) kwa gharama ya Dola za Marekani milioni tatu (TSh
bilioni 4.95)
“Tunatambua
madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi kwa Mlima Kilimnajaro. Serikali
kwa kushirikiana na jumuia za kimataifa tumekuwa tukichukua hatua mbalimbali
kuulinda,” alisisitiza Mwalimu.
Aidha,
Mwalimu alisema serikali kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii na Mamlaka
ya Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA) wametekeleza kazi ya upandaji miti na
kudhibiti uchomaji moto misitu.
Akijibu
swali la nyongeza lililoulizwa na Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini, (Chadema)
aliyetaka kauli ya serikali kuhusu kukatazwa wazee kuvuna miti yao waliyopanda
miaka 20, Mwalimu alikiri kuwapo kwa zuia hilo na kuwa taka wazee hao kuvuna
kwa kibali maalumu.
No comments:
Post a Comment