Shirika lisilo la kiserikali Resource
Oriented Development Initiative (RODI) limedhamiri kusaidia kupunguza kiwango
cha maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) mkoani Rukwa kutoka asilimia 6.2 ya
sasa hadi kufikia asilimia 2.0 ifikapo 2015.
Mkurugenzi wa RODI mkoani Rukwa, Gideon
Mpina alibainisha hayo hivi karibuni alipokuwa anazungumzia mikakati ya shirika
lake katika mapambano dhidi ya Ukimwi.
RODI inatekeleza miradi ya
mapambano dhidi ya maambukizi
ya VVU na kutoa Elimu
ya Afya ya Uzazi na Ujinsia
(TMEP) kwa ufadhili wa Taasisi ya Kimataifa
ya Elimu ya Afya na Uzazi kutoka
nchini Sweden (RFSU) ambapo
kiwango cha maambukizi ya VVU
kimeripotiwa kuongezeka
kutoka asilimia 4.9
mwaka 2010 hadi kufikia
asilimia 6.2 mwaka huu.
Alizitaja mbinu zitakazotumiwa na RODI kupunguza
maambukizi hayo ya VVU
kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia sasa
zikiwemo kusambaza kondomu
na kutoa elimu
sahihi ya matumizi yake
pia kuwaelimisha wakazi
wa mkoani humo umuhimu
wa tohara kwa wanaume.
Alibainisha kuwa
kiwango cha maambukizi wilayani Sumbawanga kinatisha
ambapo kiwango cha maambukizi katika
Mji Mdogo wa Laela na Mji wa Mpui
wilayani humo ni
asilimia 10 kila
mmoja.
Kwa mujibu wa takwimu
za Afya mkoani Rukwa,
kiwango cha maambukizi ya VVU Manispaa ya Sumbawanga kimefikia
asilimia 5.2.
No comments:
Post a Comment