Wafanyabiashara wilayani Nachingwea
mkoani Lindi wanadaiwa kutumia fedha
bandia kununulia zao la ufuta.
Hayo yalibainishwa na Mkuu wa Wilaya ya
Nachingwea, Regina Chonjo wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi.
Alisema wachuuzi hao wanaenda kwa
wakulima kununua ufuta vijijini, kuwalaghai
na kuwapa fedha za bandia bila wao wenyewe kufahamu na hatimaye
kuzipokea.
Chonjo alisema ni vyema wakulima
wakafanya mauzo ya fedha taslimu kupitia benki za NMB au CRDB kwani wao wana
mashine maalumu ambazo itawezekana kubaini uhalali wa noti hizo.
Alisema ulipwaji wa fedha hizo za
bandia kufanyika huku pia wakulima wakiwa wamelaghaiwa kwa bei ndogo ya zao
kutoka Sh 2,500 kwa kilo moja hadi kufikia Sh 1,200 katika msimu wa mwaka huu.
Mkuu huyo wa Wilaya alisema kuwa
uongozi wa Wilaya utafuatilia kwa makini matendo ya wanunuzi hao ya kuwalaghai
wakulima kwa kuwapa bei ya chini chini ya utaratibu uliokubaliwa, huku
wakiwalipa fedha feki.
No comments:
Post a Comment