Ofisa
Masoko wa Kampuni ya NN General Supplies Simon Lyatuu (47) amepandishwa
kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashitaka ya
wizi wa Sh milioni 69.8.
Lyatuu
alifikishwa mahakamani hapo jana na kusomewa mashitaka na Wakili wa Serikali
Celina Kapange mbele ya Hakimu Mkazi Gabriel Mirumbe.
Wakili
Kapange alidai kuwa kati ya Januari mosi, 2012 na Aprili 30, mwaka jana katika
kampuni hiyo iliyopo mtaa wa Gerezani barabara ya Kilwa, Lyatuu aliiba Sh
milioni 69,885, 525 mali ya mwajiri wake.
Mshitakiwa
alikana mashitaka na upande wa mashitaka ulidai
upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kuomba tarehe nyingine ya kutajwa.
Hakimu
Mirumbe alisema mshitakiwa atapata dhamana endapo atakuwa na wadhamini wawili
watakaosaini hati ya Sh milioni 20 na mmoja awasilishe hati ya mali
isiyohamishika yenye thamani hiyo.
Mshitakiwa
alirudishwa rumande kwa kuwa hakukidhi masharti ya dhamana ambapo upande wa
Jamhuri ulikwenda kuhakiki hati ya nyumba iliyowasilishwa na wadhamini wa
mshitakiwa. Kesi itatajwa tena Juni 18, mwaka huu.
No comments:
Post a Comment