Katika
kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, umetolewa mwito wa uhifadhi na
utunzaji wa mazingira kufanyika kila
siku badala ya kusubiri Siku maalumu ya Maadhimisho ya Mazingira Duniani.
Makamu
wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal alitoa ushauri huo wakati akifunga maadhimisho ya kilele cha
Siku ya Mazingira yaliyofanyika kitaifa mkoani Mwanza kwenye viwanja vya
Furahisha.
Alisema
ili kupunguza na kudhibiti athari za mabadiliko ya tabianchi zinazotishia
jitihada za kujiletea maendeleo ni muhimu kuchukua hatua za kuhakikisha mazingira yanatunzwa na kuhifadhiwa vizuri.
“Tupande
miti na kutunza misitu yetu ili itusaidie kunyonya hewa ukaa zinazosababisha
mabadiliko ya tabianchi na katika nchi zilizoendelea tutashinikiza
zichukue hatua mahususi za kupunguza
uzalishaji wa gesijoto,” alisema Dk Bilal.
Alisema
pamoja na athari za mabadiliko ya tabianchi, mazingira ni sehemu ya maisha ya
binadamu lakini wameendelea kushuhudia uharibifu mkubwa wa mazingira unaotokana
na sababu mbalimbali zikiwemo za kilimo, mifugo, viwandani, matukio ya moto na
uchomaji wa misitu na mrundikano wa taka katika maeneo ya miji na makazi.
Alisema
Tanzania imeshuhudia athari za madadiliko ya tabianchi katika sekta zote za
kiuchumi zikiwemo za kilimo, nishati, maji, miundombinu, mifugo, afya na
maliasili.
Kwa
upande wa kilimo, Makamu wa Rais alisema imeathiriwa kutokana na ukosefu wa
mvua za uhakika na ukame wa mara kwa mara unaosababisha uzalishaji hafifu wa
mazao ya kilimo hivyo kuchochea tatizo la njaa nchini nakulazimisha serikali
kuwapa chakula wananchi.
Akizungumzia
athari kwenye miundombinu alisema katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na
matukio mengi ya mafuriko ambapo kwa mwaka huu yamegharimu maisha ya Watanzania
na kuharibu miundombinu.
Alisema
katika Jiji la Dar es Salaam zaidi ya Sh bilioni 20 zinahitajika kwa ajili ya
kurejesha miundombinu ya barabara na kwamba mafuriko yaliyotokea Morogoro
yameleta hasara kubwa kwa taifa.
Waziri
wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif
Rashid alisema njia rahisi ya kupambana na ugonjwa wa homa ya dengue ni usafi
wa mazingira. Alisema wananchi wanatakiwa kushiriki kikamilifu katika kuweka
mazingira safi kwenye maeneo yanayowazunguka.
Alisema
tangu ugonjwa huo ulipuke kumekuwa na wagonjwa 1,119 na vifo vya watu wanne.
Katika
kilele cha maadhimisho hayo ya Siku ya Mazingira, zawadi na tuzo mbalimbali
zilitolewa kwa taasisi na watu binafsi walioshiriki kwenye utunzaji wa
mazingira.
No comments:
Post a Comment