Waziri
wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu amezindua awamu ya 13 ya upandaji wa Mlima
Kilimanjaro kwa lengo la kuchangia fedha za kusaidia mapambano dhidi ya ugonjwa
ya Ukimwi.
Mpango
huo uliopewa jina la Kili Challenge, unadhaminiwa na Mgodi wa Dhahabu wa
Geita kwa kushirikiana na Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) na watu
500 walipanda mlima huo.
Akizungumza
katika uzinduzi huo, Nyalandu alisema kuwa hatua ya kupanda Mlima Kilimanjaro
kwa lengo la kuchangia fedha za kupambana na Ukimwi ni nzuri kwa kuwa inaongeza
hamasa kwa wananchi katika kupambana na ugonjwa huo.
Alisema
kuwa ni hatua ambayo wahusika wanaopanda mlima huo wanakuwa wametimiza dhana ya
kutumia utalii katika kupambana na Ukimwi.
Nyalandu
alisema pia unaongeza hamasa katika kusaidia Serikali kutimiza Malengo yake ya
Milenia ya kuhakikisha kuwa hakuna maambukizi nchini hasa kutoka kwa mama
kwenda kwa mtoto.
"Hii
ni hatua nzuri kubwa na yenye tija kubwa kwa wanajamii kwa ujumla wake, kwa
kuwa hawa wapandaji mlima wanakuwa wamechangia fedha zitakazosaidia mapambano
dhidi ya Ukimwi kwa njia hii ambayo ni sehemu ya utalii,” alisema Nyalandu.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi
(TACAIDS) Fatma Mrisho alisema Watanzania kwa ujumla wanatakiwa kuungana
na kila mmoja kwa wakati wake kupambana na ugonjwa huo.
Alisema
kuwa changamoto kubwa kwa sasa ni katika kuhakikisha kuwa jamii inaondokana na
hali ya unyanyapaa pamoja na kuondoa maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa
mtoto.
Alisema
kuwa takwimu zinaonesha kuwa watu milioni 1.6 wanaishi na virusi vya Ukimwi
huku kukiwa na maambukizi mapya 86,000 kwa kila mwaka.
Akizungumza
katika sherehe za uzinduzi huo Mkurugenzi Mtendaji wa Mgodi wa Geita, Michael
Van alisema kuwa mgodi huo utaendelea kushirikiana na serikali katika
kupambana na Ukimwi.
No comments:
Post a Comment