Imani
potofu ya kuunganishwa na dini inayodaiwa kuabudu shetani (Freemason) nusura
ivuruge kazi ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf) ya kuandikisha majina ya
kaya masikini, Wilaya ya Mkalama, mkoani Singida.
Imedaiwa
kuna watu walisambaza ujumbe wa imani potofu kuwa watakaokubali kuorodheshwa
majina yao wangeunganishwa na dini hiyo inayodaiwa kuwa inaabudu shetani.
Akizungumzia
sakata hilo, Mwenyekiti wa Kijiji cha Mwanga, Ezekiel Kamunga alisema alisikia
suala hilo likizungumziwa juu juu na baadhi ya watu lakini hata hivyo hakuna
ukweli wowote juu ya suala hilo.
Alisema
ujumbe huo ulisambazwa na watu wenye nia ya kukwamisha kazi bila ya kuwa na
sababu za msingi za kufanya hivyo.
"Haya
maneno yapo ila sijahakikisha, baadhi ya watu wenye nia mbaya na chafu ya
kufanya mpango huu usifanikiwe ndiyo wamesambaza hizi taarifa lakini hazina
ukweli wowote," alisema.
Alisema
katika kazi hiyo ililenga kuandikisha kaya 366 ambapo mpaka jana walikuwa
wameshaandikisha zaidi ya kaya 150.
Kamunga
alisema baada ya kukamilika kwa kazi hiyo kutasaidia kubaini ni kaya ngapi
hazijaandikisha kutokana na vitisho hivyo na pia kumbaini aliyesambaza taarifa
hizo.
"Sasa
hivi bado tunaendelea na kazi ya kuwaandikisha, tukishamaliza ndiyo tutajua
kaya ngapi hazijaandikishwa na kumtafuta mtu aliyesambaza taarifa hizi za
uongo," alisema.
Kamunga
aliwaomba wananchi kupuuzia kauli hizo alizoziita za mtaani kwani hazina ukweli
na zinaenezwa ili kuvuruga mpango huo wenye nia ya kuwanufaisha wananchi.
No comments:
Post a Comment