Shirika
la Usafiri Dar es Salaam (UDA) limekubaliana na Mamlaka ya Usafiri wa
Nchikavu na Majini (Sumatra) kuweka vibao katika mabasi yake kuonesha njia
yanakotoa huduma na si kupaka rangi.
Mkuu
wa UDA, Hamdy Al Hadj alisema kibao kitakachowekwa, kitakuwa na rangi ya eneo
husika kama ilivyo kwa daladala nyingine.
“Kwa
mfano kama basi linakwenda Gongo la Mboto basi katika kibao kilichoko mbele ya
basi kiwe na rangi ya eneo hilo kama ilivyo katika daladala,” alisema Hamdy.
Alisema
wanaendelea kukamilisha uwekaji vibao hivyo pamoja na kuweka namba za
wamiliki kwenye magari yote ili abiria waweze kutoa taarifa watakapohudumiwa
tofauti.
“Tumeweka
namba za simu nyuma ya mabasi ili kuwasaidia abiria kutoa taarifa pindi
watakapokuwa wakipata huduma tofauti kwa mfano kupandishiwa nauli,” alisema na
kuongeza kuwa namba hizo zimesaidia kupokea malalamiko mengi ya abiria kuhusu
wafanyakazi wanaotoa huduma mbaya.
Alihimiza
abiria kusaidia kwa kutoa taarifa watakapohudumiwa isivyostahili ili madereva
au makondakta watakaokiuka utaratibu wachukuliwe hatua.
Katika
hatua nyingine, Kampuni ya Simon Group Limited imesisitiza dhamira yake
ya kuboresha Sekta ya Usafiri katika Jiji la Dar es Salaam.
“Tumeona
taarifa ambazo zimekuwa zikichapishwa katika vyombo mbalimbali vya habari
ikiwamo mitandao ya kijamii …wakijaribu kuwafanya watu waamini kila uwekezaji
unaofanywa katika kuboresha mfumo wa usafiri jijini Dar es Salaam kupitia UDA
hauna maana,” alisema Ofisa Mtendaji Mkuu, Robert Kisena kupitia taarifa
kwa vyombo vya habari.
Alisema
mpango ambao kampuni imedhamiria kuboresha huduma ya usafiri Dar es Salaam, uko
pale pale ukihusisha mradi wa kuwa na mabasi zaidi ya 3,000 pamoja na mabasi
mengine ya kifahari 50 yenye viyoyozi na huduma ya intaneti.
Alisema
kwamba tathmini inaonesha kuwa ili kuwezesha mabasi yapatayo 3,000 kufanya kazi
hapo baadaye wataalamu wapatao 7,800 watahitaji kupewa mafunzo na kuajiriwa.
Aliongeza
kwamba mara baada ya mpango huo kukamilika, unyanyapaa miongoni mwa wanajamii
kuhusu utumiaji wa mabasi ya uma hautokuwepo tena na watu wataacha kupaki
magari yao katikati ya Jiji, watanunua tiketi za UDA kwa njia ya mtandao.
“Ninataka
kuwahakikishia Watanzania wote na wale wanaoendelea na kampeni zao kwamba
mpango wa UDA kuboresha mfumo wa usafiri Dar es Salaam ni jambo linalowezekana,
Tutafanya kazi kwa karibu na Serikali pamoja na Jiji ili kuona wakazi wa Dar es
Salaam wanapata huduma rahisi na ya uhakika ya usafiri,’’ alisema Kisena.
No comments:
Post a Comment