Safu
mpya ya uongozi wa Taifa ya Chama cha Wananchi (CUF) inatarajiwa kupatikana
mwezi huu katika uchaguzi utakaofanyika wiki ijayo, jijini Dar es Salaam.
Chama
hicho kinachoongozwa na Mwenyekiti, Profesa Ibrahim Lipumba, Makamu wake,
Machano Khamis Ali na Katibu Mkuu, Seif Sharif Hamad, kitafanya mkutano
wake mkuu Juni 23 hadi 27 utakaokwenda sanjari na uchaguzi wa viongozi.
Akizungumza
jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu, Hamad alisema maandalizi yote ya msingi
kwa ajili ya mkutano huo yamekamilika.
Alisema
watawachagua viongozi wakuu wa kitaifa wa chama hicho ambao ni Mwenyekiti wa
Taifa, Makamu Mwenyekiti na Katibu Mkuu.
Viongozi
wengine watakaochaguliwa katika mkutano huo ni wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi
Taifa pamoja na wajumbe wa Viti Maalumu vya Wanawake.
Alisema
katika mkutano huo, wajumbe watapokea taarifa mbalimbali za kazi za chama
kuanzia mwaka 2009 hadi 2014 ambapo pia watapata fursa ya kuzijadili.
Kwa
mujibu wa Hamad, chama kinaendelea na vikao mbalimbali kikiwemo cha Kamati ya
Utendaji, ikiwa ni maandalizi ya mwisho kwa ajili ya mkutano huo kabla ya
wajumbe kuwasili kwa ajili ya mkutano huo wa kitaifa.
No comments:
Post a Comment