Mtoto
Jeremiah Nyamuhanga (2) mkazi wa Machimbo amekufa baada ya kutumbukia kwenye
kisima cha maji karibu na nyumbani kwao.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi alisema, mtoto huyo alitumbukia juzi
saa 10 jioni katika eneo la Machimbo, Kitunda, Wilaya ya Ilala.
Alisema
maiti yake ilikutwa ikielea ndani ya kisima hicho kilicho karibu na nyumba yao.
Inasadikiwa mtoto huyo alimtoroka baba yake aliyekuwa kwenye banda la kuku na
kwenda kucheza ambapo alitumbukia ndani ya kisima hicho.
Maiti
ya mtoto huyo amehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na upelelezi
unaendelea.
Katika
tukio jingine, abiria wa pikipiki ambaye bado hajafahamika amekufa baada ya
pikipiki aliyokuwa amepanda kugonga lori kwa nyuma.
Kamanda
Minangi alisema ajali hiyo ni ya juzi saa 5 asubuhi katika Barabara ya Pugu
eneo la Mombasa.
Alisema
pikipiki aina ya Lingken yenye namba T116 CTF iliyokuwa ikiendeshwa na mtu
asiyefahamika akitoka Mombasa kwenda Gongo la Mboto, akiwa amempakia abiria
asiyefahamika mwanamke anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 40 na 45
aligonga kwa nyuma lori aina ya Scania lenye namba T743 lililokuwa likiendeshwa
na Charles Yusuph (35).
Katika
ajali hiyo ambapo wote walikuwa katika uelekeo mmoja, abiria huyo alikufa papo
hapo na maiti imehifadhiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili na jitihada za
kumtafuta dereva wa pikipiki aliyekimbia baada ya ajali zinaendelea, huku
pikipiki ikiwa imehifadhiwa Kituo cha Polisi Stakishari.
No comments:
Post a Comment