Halmashauri
za Jiji la Dar es Salaam zimeaswa
kushirikiana na Serikali za Mitaa kusimamia sheria ya utunzaji wa
mazingia ili kufikia malengo ya kuimarisha usafi.
Kaimu
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sophia Mjema aliyasema hayo jana jijini wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mazingira
ambayo kitaifa yamefanyika jijini Mwanza.
Maadhimisho
hayo huadhimishwa Juni 5, kila mwaka, yameanza rasmi Juni Mosi mwaka
huu yenye kaulimbiu ‘’Utunzaji wa
mazingira kukabili mabadiliko ya tabia ya nchi.’’
Alisema
sheria hizo zinapaswa zisimamiwe ili kuzuia wanaojenga nyumba kwenye kingo za
mito ambazo zinasababisha maji kushindwa kupita katika njia zake na kusababisha
mafuriko.
Aidha, aliwataka kuzuia utiririshaji wa majitaka
kwenye mitaro ya barabara na makazi ya watu wakati wa mvua, kwani wanahatarisha
maisha na badala yake kutafuta magari ya
majitaka kuondoa uchafu huo.
‘’
Tunaendelea kusisitiza kwamba Jiji la Dar es Salaam hakuna machimbo ya mchanga
wala vifusi hivyo viongozi wa Serikali za Mitaa wasimamie kwani chanzo cha
kubomoka kwa madaraja yanaleta maafa kutokana na uchimbaji,’ ’alisema Mjema.
Aliongeza
kuwa watendaji wazuie wafanyabiashara walio katika hifadhi za barabara kwa kuwa
maeneo hayo si salama na kwamba waende maeneo waliyoandaliwa na Serikali.
Alisema lazima kutambua mabadiliko ya tabia ya nchi
ambayo yameongezeka kutokana na shughuli za binadamu hivyo kutafuta njia ya kutatua matatizo
yatokanayo na mabadiliko hayo.
Naye,
Mwenyekiti wa Taasisi isiyo ya kiserikali inayoshughulikia masuala ya
mabadiliko ya hali ya hewa (Forum cc), Euster Kibona alitoa mwito kwa viongozi
wa Mkoa kutoa kipaumbele kwa taasisi hizo kupambana na mabadiliko ya tabia ya
nchi.
Alisema
wanajamii wanahitaji kutoa ushirikiano katika kukabiliana na tatizo hilo kwa
kudhibiti uzalishaji mkubwa wa taka na matumizi ya kuni kwa vijijini.
‘’Elimu
ya ziada inatolewa kuhusu matumizi ya kuni licha ya matumizi ya gesi kuwa juu hivyo tunaiomba
Serikali iangalie jinsi ya kudhibiti gharama za gesi kuwasaidia wengine kuepuka
ukataji wa miti,’’ alisema Kinabo.
No comments:
Post a Comment