Jumuiya ya Mabohora
nchini Tanzania inatarajiwa kupanda miti kesho jijini Dar es
Salaam.
Akizungumzia
shughuli hiyo, Seifeddin Jamali ambaye ni mmoja wa watendaji wa jumuiya hiyo, alisema shughuli hiyo
itawakilisha siku ya upandaji miti
duniani inayoratibiwa na Jumuiya ya Mabohora ulimwenguni kote.
Alisema,
jumuiya hiyo huadhimisha siku ya upandaji miti kila ifikapo Juni 2 ya kila
mwaka kote waliko wanajumuiya ikiwemo Tanzania.
Alisema kwa
mwaka huu watashirikiana na Manispaa ya Ilala kwa ajili ya kulifanya jiji la Dar es Salaam kuwa la kijani.
Alisema, eneo
litakalohusika ni la Uwanja wa Ndege jirani na kiwanda cha Bakhressa ambapo jumla ya miche 1,252 itapandwa.
Alisema,
miche hiyo ni ya aina mbalimbali ikiwemo jamii ya mitende na
itapandwa katika maeneo mengi ya wazi
ikiwemo kando kando na eneo la
katikati la Barabara ya Nyerere.
Aliongeza
kuwa, pamoja na watu mbalimbali, shughuli hiyo itahudhuriwa pia na Meya wa
Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa na baadhi ya watendaji wake.
Alitoa mwito
kwa wakazi wa maeneo jirani kuungana na
wanajumuiya na Manispaa ya Ilala katika zoezi hilo la upandaji miti likaloanza
saa tatu asubuhi.
No comments:
Post a Comment