Katibu Mkuu wa
Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad amerejesha fomu ya kugombea
tena nafasi ya Katibu Mkuu wa chama hicho, na kusisitiza msimamo wake wa
kuendelea kuwaunganisha Wazanzibari.
Aidha, amewataka
wanachama wengine wenye `ubavu’ wa kuchuana naye katika nafasi hiyo wajitokeze,
akisema nafasi anayowania haina mwenyewe, licha ya kuwa ameishikilia kwa muda
mrefu, tangu kuasisiwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa mwanzoni mwaka 1992.
Akikabidhi
fomu yake kwa Katibu wa CUF Wilaya ya Magharibi Unguja, Juma Rajab, Maalim Seif
alesema suala la ubaguzi kamwe halitopewa nafasi ndani ya chama hicho.
Aliongeza
kuwa, Wazanzibari wote ni wamoja bila ya kujali asili ya mtu anapotokea ndani
ya visiwa vya Zanzibar, na kuhimiza umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi.
Maalim Seif
ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, amerejesha fomu hiyo baada
ya kuamua kuingia tena kwenye kinyang’anyiro hicho na kuchukua fomu Ijumaa
iliyopita, ambapo alisindikizwa na viongozi wa CUF na wafuasi kadhaa wa chama
hicho.
No comments:
Post a Comment