LEO NI MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIA



Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Dk. Binilith Mahenge leo atafungua maadhimisho ya siku ya Mazingira dunia yatakayofanyika kitaifa katika mkoani hapa.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Kaimu Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Baraka Konisaga alisema maadhimisho hayo yatafanyika kwenye uwanja wa Furahisha, jijini hapa ambapo hadi kilele chake Juni 5, mwaka huu wageni kutoka ndani na nje ya nchi wanatarajiwa kushiriki.
Alisema katika maadhimisho hayo yenye kaulimbiu ya 'Tunza mazingira ili kukabiliana na tabia nchi' inahimiza juu ya umuhimu wa uhifadhi wa mazingira kutokana na mabadiliko ya tabia nchi kuwa na changamoto mbalimbali katika taifa.
Alisema katika maadhimisho hayo shughuli mbalimbali zitafanyika ikiwa ni pamoja na kufanya usafi, kuhamasisha wananchi kuhusu utunzaji wa mazingira kwa njia ya makongamano, kupanda miti, kuzoa takataka, kuondoa magugu maji katika ziwa Victoria na ufugaji wa nyuki.
Naye Naibu Katibu mkuu ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Anjelina Madete alisema mabadiliko ya tabia nchi yamesababishwa na ges joto ambazo hutokana na shughuli za maendeleo kama vile viwanda ambazo zimeongezeka kwenye uso wa dunia.
Alisema mabadiliko hayo yameleta athari mbalimbali zikiwemo za kutotabilika kwa majira ya mvua,kutishia visiwa kutoweka, maeneo ya misitu mikubwa kupungua kutoka na na bionuai.

No comments: