Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga, Mathew Sedoyeka amepongezwa na
vijana wilayani humo kwa uamuzi
wake wa kuwapiga
marufuku vijana wote
wa kiume popote wilayani humo
kuvaa suruali kwa mtindo wa
mlegezo maarufu kama Kata K .
Hata hivyo wamemtaka
DC huyo apige marufuku
wasichana kuvaa mavazi
yasiyo ya staha
ikiwemo vipedo na
sketi fupi huku
baadhi yao wakiwa nusu
uchi kwamba uvaaji
huo nao pia hauendani na
maadili ya Watanzania.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na mwandishi wa habari
hizi baadhi ya vijana wa
kike na kiume wamemtaka Mkuu huyo wa Wilaya, kuamuru
kuwa kijana yeyote
akikamatwa amevaa mavazi
hayo yasiyo na stahi awe wa
kike au
wa kiume atozwe faini ya
kiasi cha Sh 50,000 na fedha hiyo apewe
mtu aliyemkamata na kufikishwa Kituo
cha Polisi.
"Kwa staili hii ya kupigwa faini itatuogopesha
na nikuhakikishie tutaacha
tabia hii ya kuvaa kiajabu ajabu," alisema Tofilo Mbalamwezi, mkazi wa eneo
la Majengo.
Kauli
na pongezi hizo za vijana
hao zimekuja siku
chache baada ya DC kupiga marufuku uvaaji wa suruali kwa staili
ya Kata K kwa kijana yeyote wa
kiume mahali popote wilayani humo.
Pia Sedoyeka aliwaagiza viongozi wa
serikali za mitaa, vijiji, kata tarafa na wilaya kushirikiana na Kamati za
Ulinzi na Usalama katika maeneo yao ya kiutawala kuwachukulia hatua kali vijana
wote wa kiume watakaobainika kuvaa suruali zao kwa staili hiyo ya Kata K.
Alitoa maagizo hayo hivi karibuni
akihutubia mikutano mbalimbali ya hadhara wilayani humo ambapo alisema tabia hiyo ya vijana wa kiume kuvaa
suruali zao kinyume cha utaratibu haiwezi kuvumilika kwa kuwa inatukanisha
jamii.
No comments:
Post a Comment