Kampuni ya simu za mkiononi ya Vodacom imendelea na azma yake ya
kuhakikisha inawafaidisha wateja wake kupitia huduma zake, huku wakitengeneza
nafasi za ajira kupitia maduka yake yanayoendelea kufunguliwa nchi nzima.
Akizundua duka jipya la Vodacom jijini Dar es Salaam, Mkuu
wa Idara ya Mauzo ya Rejareja, Upendo Richard alisema dhamira kubwa ya
kusambaza maduka ya kampuni hiyo ni kusogeza na kuboresha huduma kwa wateja
popote walipo lakini pia kutengeneza nafasi za ajira.
Duka hilo ambalo liko Sinza Afrika Sana ni la 18 kwa wilaya
ya Kinondoni pekee na la 79 Tanzania nzima. "Ajira hizi kwa namna moja au
nyinigine ni suluhu la upungufu wake nchini na pia hupunguza mzigo kwa serikali
katika jitihada za kuhakikisha watu wanajiajiri wenyewe."
Alisema kwa kila duka la Vodacom linalofunguliwa, watu
watano mpaka saba huajiriwa kwa nafasi mbalimbali na akasema kuwa takribani watu
400 wameajirwa katika maduka hayo kama
meneja wa duka, uhasibu, wauzaji simu, watoaji ushauri kwa wateja pamoja
na wakala wa M-Pesa.
"Wateja wote wa Vodacom sasa wasipate tabu za kwenda
maeneo ya mbali kutafuta huduma za kimawasiliano, badala yake watumie duka hili
lililopo hapa Sinza Afrika Sana." Alisema
Richard na kuongezea, "Huduma zinazotolewa hapa ni sawa na maduka
mengine ili kuweza kutimiza haja zao na kuepukana na usumbufu wa kwenda mbali."
Naye mteja wa kwanza kutumia duka hilo mara baada ya
kufunguliwa rasmi, Alfred Joseph, ambaye ni mkazi wa Sinza Afrika Sana ameishukuru
Vodacom kwa jitihada zao za kusogeza huduma kwa wateja na kuwapunguzia usumbufu
wa kusafiri umbali mrefu.
No comments:
Post a Comment