Serikali
ya Tanzania imepata mkopo wa Sh bilioni 24.1 kutoka Serikali ya Japan ikiwa ni
sehemu ya kuisaidia bajeti yake.
Waziri
wa Fedha, Saada Mkuya Salum na Balozi wa Japan nchini, Masaki Okanda walitia
saini mkataba wa mkopo huo. Salum alisema fedha hizo zitasaidia katika
maeneo muhimu ikiwemo afya, maji na nishati.
Mkuya
alisema fedha hizo kwa kiasi kikubwa zitatumika katika kupambana na umasikini.
Alisema
juhudi kama hizo zimeimarisha huduma muhimu kwa jamii na kupunguza umaskini
katika maeneo mengi ambapo kulingana na ripoti ya sensa ya watu na makazi
iliyotolewa hivi karibuni, kiwango cha umasikini kwa Watanzania kimepungua na
kipato cha Mtanzania kinapanda.
Kwa
upande wake, Balozi wa Japan nchini, Okada alisema mkataba huo ni wa
ushirikiano wa pamoja na Benki ya Dunia na kwa masharti nafuu ya riba ya
asilimia 0.01.
Alisema
msaada huo hutolewa kulingana na bajeti ya serikali na fedha hizo hulenga
utekelezaji wa juhudi za kupunguza umasikini zinazofanywa na serikali ya
Tanzania, hususan Mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini (Mkukuta).
Balozi
huyo alisema serikali ya Japan iko tayari kuongeza msaada kwa Tanzania kufikia
malengo ya kuchangia maendeleo ya miundombinu ya barabara, reli, nishati na
viwanda.
No comments:
Post a Comment