Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Hawa Ghasia amesema mipango
miji si kupima viwanja pekee kama inavyofanywa sasa bali ni kuzingatia mahitaji
mengine ya jamii kwa ajili ya maendeleo.
Ghasia alitoa kauli hiyo jana jijini
Dar es Salaam kwenye kongamano kuhusu uendelezaji wa mipango miji na majiji kwa
maendeleo endelevu lilioandaliwa na taasisi ya Uongozi Institute.
Alisema halmashauri nyingine zimekuwa
na dhana ya kupanga miji wa kuangalia upimaji wa viwanja vya makazi pekee na
kusahau huduma nyingine zilizomuhimu kwa jamii.
'Mipango miji si kupima viwanja vya
makazi peke, ni lazima kuzingatia maeneo ya viwanda, burudani na hata sehemu ya
kupumzishwa pindi maisha yetu hapa duniani yanafikia mwisho,' alisema.
'Kwa sasa upangaji miji unaendana
kivyake na mipango ya maendeleo inaenda kivyake. Tutafakari jinsi ya kupanga
miji yetu vizuri,' alisema.
Ghasia alisema miji na majiji
iliyopangwa vizuri ina uwezo wa kutoa huduma nzuri kwa wananchi.
Aidha, Ghasia alipongeza hatua ya
kuwashirikisha mameya wa miji na majiji badala ya hali ya sasa ya kushirikisha
wataalamu na wakurugenzi pekee ambao wamekuwa wakihama kila siku.
"Pamoja na meya ni mwanasisasa
lakini ni mwananchi wa eneo hilo, hivyo kama hatakuwa madarakani atakuwa
mwananchi ambaye kama atashirikishwa, basi ni rahisi kufahamu mipango ya miji
iliyopo," alisema.
Ghasia aliwataka aliwataka washiriki wa
kongamano hilo kutoka halmashauri na manispaa za miji na majiji, wataalamu wa
mipango miji wahandishi wa izara pamoja na watafiti kutoka ndani na nje ya nchi
kutoa mawazo chanya ili kuboresha hali ya miji na majiji nchini.
Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya Uongozi, Profesa
Joseph Semboja alisema sekta ya ardhi haijatazamwa vizuri na kushauri
kubadilishwa kwa sheria za upangaji mijikuanzia ngazi ya taifa hadi ile ya
nchi.
No comments:
Post a Comment