Kamati ya
Bajeti ya Bunge la Jamhuri ya Muungano, jana ilianza vikao vya siku sita
na Serikali ili kutayarisha Bajeti Kuu ya Serikali, ambayo itasomwa Juni 12,
mwaka huu na Waziri wa Fedha, Saada Salum Mkuya.
Hatua hiyo ni ya
mara ya pili kwa Serikali na Bunge kukaa pamoja kutengeneza Bajeti Kuu ya Serikali,
ambapo mara ya kwanza ilianza katika Bunge la Bajeti la mwaka jana.
Hali hiyo ni
tofauti na miaka iliyopita, ambapo Bajeti Kuu ya Serikali, ilikuwa inatayarishwa
na Serikali peke yake.
Taarifa hiyo
ilitolewa bungeni mjini hapa jana na Spika wa Bunge, Anne Makinda alipokuwa
akielezea ratiba ya shughuli za Bunge hadi sasa.
“Zile siku 26 za
kujadili wizara zimekwisha jana. Katika siku zote hizo tulikuwa tunajadili
sekta moja moja, lakini leo (jana) hadi
tarehe 11
Juni Kamati ya Bunge itajadiliana na Serikali kwa undani zaidi juu ya
utekelezaji wa bajeti ya sasa na utayarishaji wa bajeti kuu ijayo.
Kipindi hiki
Bunge linashiriki katika kutengeneza Bajeti ya Serikali,” alisema Spika.
Alieleza kuwa
majadiliano hayo, baina ya Serikali na Kamati
ya Bajeti,
yatahusisha pia wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge.
Spika alitaja
wizara ambazo Wizara ya Fedha, itajaribu
kutafuta fedha katika vyanzo vyake mbalimbali kukamilisha bajeti za
wizara hizo.
Kuwa ni Wizara
ya Maji, Wizara ya Nishati na Madini na Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na
Teknolojia.
No comments:
Post a Comment